Raia 50 wameuwawa Mosul, Iraq



Watu 50 wameuwawa,nchini Iraq wakati pale wakiukimbia mji huo kwa ajili ya kunusuru maisha yao, dhidi ya mapigano mabaya yanayotekelezwa na wanamgambo wa Islamic State.
Wanahabari wa runinga ya Reuters, wamepata maiti ya wanaume, wanawake na watoto, zikiwa zimetapakaa katika barabara za mji huo.
Hilo limetokea katika Wilaya ya Zanjili, karibu na eneo la mapigano, ambapo jeshi la taifa ya Iraq, linakabiliana vikali na wanamgambo hao wa Dayesh, kama wanavyofahamika.
Mfanyakazi mmoja wa shirika la utoaji misaada la Marekani- Dave Eubank, amesema kuwa wapiganaji wa I-S, wamekuwa wakiwamiminia risasi wananchi wanaojaribu kuutoroka mji huo.
Amesema kuwa ameona maiti 50, lakini kwa msaada wa jeshi la Marekani linalosaidiana na wanajeshi wa Iraq, amefaulu kuwaokoa watu wawili tu.
Raia 50 wameuwawa Mosul, Iraq Raia 50 wameuwawa Mosul, Iraq Reviewed by KUSAGANEWS on June 04, 2017 Rating: 5

No comments: